Maisha


Maisha ni muda wa kukutana na shida.
Kwa hio, ukipata chakula na soda
Usitafute vitu vingine
Tena kama wewe ni mwembamba, usitake kua mnene.

Lakini tena, usitazame mbele,
Hangalia karibu na we, furahi kwa kitu chochote umesha pata tena piga vigelegele
Badala ya kufikilia kuhusu maisha ya kesho au kulia na kupiga kelele.

Usiogopi maisha
Kwa sababu chini, vitu vyote vitaisha.
Jua kwamba, ijapokuwa maisha ni magumu
Ukipata mazuri, hayatapotea kama gurudumu.

Usitafute kushikana mieleka na maisha
Ili ubute shida zinazokusumbua kuishiwa au kuisha
Wala usitumie nguvu zako ili upate uzima
Lakini ni lazima
Ufanye kila kitu kwa imani, yaani akili
Tena kabla ya kuitikia, fikili
Kwa hio, utapata kitu chochote unachotaka
Kwa sababu umetumia akili kali kama sungura alikuwa anadanganya paka.

Ndugu yangu, mimi ni mtungaji wa mashairi
Kukwambia ukweli sio siri.
Ninataka nikwambie kwamba maisha ni noma.
Kila siku kila mutu mzima na kilema
Huamuka alfajiri
Wakaenda kupigana na maisha pia wakakutana na shida tofauti
Lakini wanyama na wadudu hawaatii wasiwasi kukusu maisha, hivyo hivyo inavyofanya miti

Mwenzangu, jua kwamba maisha ni kama uwanja wa vita
Kila muda ni kupigana na tabu tofauti na kuendelea kutafuta
Kupata bahati ya kuisha mda mdogo
Na kuondoa kidogo
Shida zinazotuzingatia dimbwi ya maovu
Ili tuwe werevu
Tuonekane kavu.

Maisha si kitu cha kupatwa ovyo au kinyume cha sheria
Maisha ni kitu kinachopangwa na kucheka na kulia

Maisha ni kutembea, kuporomoka, kuanguka na kusimama
Maisha ni ushujaa wa kutafuta kuwa salama.





 _Artist Poet Boshir Melcky


Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

Où est allé votre amour scolaire?

La poésie au Burundi

Ma perle rare